Mjue Bi Khadija binti Khuwailidi mke wa kwanza wa Mtume
MFAHAMU: K HADIJA BINT KHUWAILYD MKE WA KWANZA WA MTUME MUHAMMA D: Bibi Khadijah Bint Khuwaylid (R.A) alikuwa ni mwanamke bora kuliko wanawake wote wa wakati wake. Alikuwa ni binti ya Khuwaylid Bin Asad Bin Abd il-'Uzza Bin Qusayy Bin Kilab kutokamana na Quraysh. Kabla ya Uislamu, alikuwa akiitwa atTwaahira (msafi). Khadijah alikuwa ni mwanamke tajiri, hivyo basi, akamuajiri Mtume (S.A.W) kuisimamia biashara yake ya msafara kuelekea Sham. Baada ya kushuhudia uaminifu wake na usimamizi mzuri, Bibi Khadijah alijitolea nafsi yake ili aolewe na Mtume (S.A.W), Mtume akakubali kumuoa. Kabla ya kuolewa na Mtume (S.A.W), aliolewa na Abu Halah Bin Zurarah at-Tamimi, kisha akaolewa na 'Atiq Bin 'Abid Bin 'Abdillah Bin 'Umar Bin Makhzum. Mtume (S.A.W) alipomuowa Bibi Khadijah,Mtume alikuwa na umri wa miaka ishirini na tano nae Bibi Khadijah alikuwa na miaka arubaini. Alimzalia Mtume (S.A.W) wato